Je, unatafuta nyumba ya kupanga? Unahitaji duka au ofisi kwa ajili ya biashara yako? Au labda una nyumba, chumba au jengo la kupangisha?
Karibu kwenye mfumo mpya kabisa, uliobuniwa na vijana wa Kitanzania kwa ajili ya kusaidia jamii yetu kupata makazi kwa urahisi, haraka na kwa uwazi mkubwa
Kupitia mfumo wetu, unaweza:
Kutafuta nyumba za kupanga kulingana na mahitaji yako (eneo, bei, ukubwa n.k.)
Kupata maduka au majengo ya kibiashara
Kuunganishwa moja kwa moja na wamiliki wa nyumba au mawakala walioaminika
Kuweka alert ili tukutaarifu mara tu nyumba inayokufaa inapotokea!
Kama wewe ni mmiliki wa nyumba au jengo, unaweza:
Kupakia taarifa za nyumba zako kwa urahisi kabisa
Kupata wapangaji waliothibitishwa na wenye nia ya kweli
Kufuatilia maombi, mawasiliano na miamala yote kwa usalama
Mfumo wetu si tu kutafuta na kupangisha — ni mahali ambapo wahitaji na wapangishaji hukutana moja kwa moja. Hakuna usumbufu, hakuna ulaghai. Kila kitu kiko wazi, salama, na rahisi kutumia
Tembelea tovuti yetu / app
Jisajili kama mpangaji au mpangishaji
Anza kutafuta au kupakia nyumba zako
Wasiliana na wapangaji au wamiliki kwa urahisi
Tuna timu ya msaada inayopatikana muda wote kukusaidia. Unaweza kuwasiliana nasi moja kwa moja kupitia WhatsApp, simu au barua pepe. Tupo kwa ajili yako!
Tuungane pamoja kuleta mapinduzi ya makazi Tanzania. Hakuna tena kulipia madalali wasioaminika. Hakuna tena kuhangaika mtaani bila mafanikio.